Dkt.Biteko aipongeza TMA kwa kutoa huduma bora za utabiri wa hali ya hewa

DODOMA-Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati,Mheshimiwa Dkt. Doto Biteko ameipongeza Mamalaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kwa kuendelea kutoa huduma bora za hali ya hewa nchini.
Amesema hayo Juni 3,2024 wakati alipotembelea banda la TMA kwenye ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Mazingira Duniani yanayofanyika katika viwanja vya JICC jijini Dodoma.

Dkt. Biteko alikuwa mgeni rasmi wa ufunguzi wa maadhimisho hayo muhimu kwenye ukuaji wa sekta ya mazingira nchini na alitembelea banda la TMA na kupokelewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania, Dkt. Ladislaus Chang’a.

“Hongereni sana kwa huduma bora za utabiri mnazotoa kila siku na zinatusaidia sana, hongereni sana,”amesema Dkt. Biteko.

Kwa upande wake,Dkt. Chang’a aliwaomba wananchi wa Dodoma na wale wa mikoa ya jirani watumie fursa hii kwa kutembelea banda la TMA kwenye maadhimisho haya ili kujifunza masuala mbalimbali ya mazingira na masuala mbalimbali ya hali ya hewa na huduma zitolewazo na TMA.

“Karibuni wananchi wote katika banda la TMA, mje kujifunza na kuongeza uelewa wa huduma za hali ya hewa na matumizi yake katika sekta zote za kiuchumi na kijamii. Kujifunza uhusiano wa hali ya hewa na mazingira yanayotuzunguka. Tunao wataalam bingwa wa hali ya hewa na wapo tayari kutoa elimu,” amesema Dkt. Chang’a.

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania inashiriki kikamilifu katika Maadhimisho ya wiki ya Mazingira kwa mwaka 2024 yenye kauli Mbiu "Urejeshwaji wa Ardhi, Ustahimilivu wa Hali ya Jangwa na Ukame."

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news