Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo Juni 16,2024

DAR-Balozi wa zamani wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika nchi za Canada na Jamhuri ya Watu wa China na Mhariri maarufu wa vyombo vya habari nchini, Ferdinand Kamuntu Ruhinda amefariki dunia usiku wa kuamkia Juni 15,2024.
Ruhinda ambaye aliwahi kuwa Mhariri Mtendaji wa magazeti ya CCM ya Uhuru na Mzalendo, na yale ya Serikali ya Daily News/Sunday News na Habari Leo kwa nyakati tofauti, atazikwa Juni 17, 2024 kwenye makaburi ya Kondo yaliyopo Kunduchi jijini Dar es Salaam.

Ruhinda alikuwa mwanzilishi wa magazeti ya Mwananchi na Redio Uhuru na amefariki baada ya kuugua kwa muda mrefu akikakabiliwa na maradhi ya kisukari.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news