Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo Juni 22,2024

DAR-Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umeanza zoezi la kuwaondoa wadaiwa sugu walioshindwa kutekeleza matakwa ya mkataba wa ununuzi wa nyumba katika miradi yake ya Dar es Salaam. Zoezi la kuwaondoa wadaiwa sugu hao lilifanyika tarehe 18 Juni 2024 katika mradi wa nyumba za Kijichi, Temeke.
Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Meneja Miliki wa NSSF, Geofrey Timoth amesema zoezi la kuwaondoa wadaiwa sugu walioshindwa kulipa madeni yao ya muda mrefu katika nyumba za NSSF ni endelevu katika miradi yote.

Timoth amesema kuwa NSSF ilitoa notisi ya siku 30 na baadaye ilitoa siku 14 ya kuwataka wadaiwa hao kulipa madeni yao lakini hawakulipa, hivyo baada ya kujiridhisha na kufanya tathimini, NSSF ilifanya maamuzi ya kuwatoa wadaiwa sugu katika nyumba zake ili kutoa fursa kwa wananchi wengine kununua nyumba hizo kwa utaratibu wa mpangaji mnunuzi.


Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news