Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo Juni 24,2024

IRINGA-Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imepongezwa kwa kuendeleza jitihada mbalimbali za kuboresha miundombinu katika Sekta ya Utalii nchini ambapo kwa sasa kupitia Mradi wa REGROW inatekeleza ujenzi wa Kituo cha Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) Kihesa Kilolo mkoani Iringa kitakachosaidia hifadhi za Ukanda wa Nyanda za Juu Kusini.
Mhandisi Mshauri na Meneja wa mradi huo wa ujenzi wa kituo hicho cha TAWIRI,Wilfred Saitoria amebainisha kuwa juhudi anazozifanya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan zinapaswa kuendelezwa na wao kama watekelezaji wanamuunga mkono Mhe. Rais kwa kuhakikisha wanatekeleza ujenzi huo kwa weledi ambapo mradi huo mpaka kukamilika kwake utagharimu zaidi ya shilingi bilioni moja.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news