Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo Juni 27,2024

DODOMA-Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mheshimiwa Mohamed Mchengerwa amesema Ofisi ya Rais-TAMISEMI haitasita kuchukua hatua kwa kiongozi yeyote anayewanyanyasa wananchi kupitia ukusanyaji wa ushuru wa mazao, kwani Serikali imeshatoa miongozo kuhusu ukusanyaji wa ushuru wa mazao.
Mheshimiwa Mchengerwa ameyasema hayo Juni 26,2024 wakati akichangia hoja yake bungeni jijini Dodoma katika Bunge la Bajeti ya mwaka 2024/2025 linaloendelea.

“Yapo maeneo ambapo tunaona kuna hitilafu katika ukusanyaji wa ushuru wa mazao, tutafika huko katika halmashauri zenye changamoto hizo, maelekezo yangu watanzania wasiyanyasike kwenye maeneo yao na TAMISEMI hatutasita kuchukua hatua kwa kiongozi yeyote anayewanyanyasa Watanzania katika maeneo yetu,kwani Serikali ilikwisha kutoa muongozo.”

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news