Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo Juni 28,2024

GEITA-Serikali kupitia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imefanikiwa kufikia halmashauri zaidi ya 60 nchini katika utekelezaji wa Mradi wa Uboreshaji Usalama wa Milki za Ardhi (LTIP). Utekelezaji wa mradi huo unahusisha utambuzi wa kila kipande cha ardhi, upangaji wa maeneo yote yaliyotambuliwa kwa kuandaa michoro ya mipango miji, upimaji wa viwanja vilivyopangwa kwa kuweka alama za upimaji na kuandaa ramani za upimaji na wananchi kumilikishwa maeneo yao kwa kupewa hatimilki.
Katika Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe mkoani Geita hatimiliki zisizopungua 30,827 zitatolewa kwa lengo la kuboresha milki za ardhi za wananchi ili kuchochea maendeleo ya Wilaya, kuleta usalama wa milki za ardhi, kukukuza uchumi na kupunguza au kumaliza migogoro itokanayo na ardhi.

Hayo yamebainishwa Juni 27,2024 na Mkuu wa Wilaya ya Bukombe,Mhe. Paskasi Muragili wakati wa ufunguzi wa kikao cha kujadili utekelezaji wa mradi wa LTIP katika Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news