Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo Juni 10,2024

DAR-Rais wa Young Africans Sports Club (Yanga),Mhandisi Hersi Said amewahakikishia wanachama na mashabiki wa klabu hiyo kwamba, msimu unaokuja utakuwa bora kwa klabu na benchi litakuwa imara kuliko msimu uliopita huku wachezaji wakiongezewa nguvu.

Ameyasema hayo Juni 9,2024 katika Mkutano Mkuu wa Yanga uliofanyika jijini Dar es Salaam ambapo msimu ujao wanatarajia kutumia zaidi ya shilingi bilioni 20.



"Tulifanikiwa kurejea hatua ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya miaka 25, watu wengi walidhani kuwa hatutaweza kufika hatua ya robo fainali kwa sababu tulikuwa kwenye kundi gumu sana, lakini tukawashangaza wale waliotukatia tamaa.

“Tulifanikiwa kutinga hatua ya robo fainali na kutolewa kwa matuta na Bingwa wa AFL na kigogo wa soka Afrika Kusini, Mamelodi Sundown, hata hivyo katika mchezo tulifunga bao halali ambalo Rais wa Soka Afrika, Dkt. Patrice Motsepe amenukuliwa akisema kuwa lilikuwa goli halali."



Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news