NA GODFREY NNKO
TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imesema, inathamini mchango wa watu wenye ulemavu katika ushirikiano wao wa mara kwa mara hususani wakati wa michakato ya uchaguzi nchini.
Hayo yamesemwa leo Juni 11, 2024 katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam na Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufaa Mheshimiwa Mwanaisha Kwariko wakati akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa tume, Mheshimiwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Jacobs Mwambegele.

"Tume inathamini sana mchango wenu,kwa kuwa ni sehemu ya mafanikio ya kile tulichokusudia kuwaeleza leo.
"Pia, tunawashukuru wawaklishi wa watu wenye ulemavu kwa jinsi ambavyo mmekuwa mkitupa ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu ya tume hasa katika michakato ya uchaguzi.
"Tume inatarajia kupata ushirikiano mkubwa zaidi kutoka kwenu, kwa kuwafikishia wananchi taarifa sahihi na kwa wakati zinazohusu zoezi lililopo mbele yetu la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na kuwahamasisha wananchi kujiandikisha kuwa wapiga kura."

"Kwa hiyo, tume imekuwa na utaratibu wa mara kwa mara wa kuwashirikisha wadau mbalimbali katika utekelezaji wa majukumu yake, kikao hiki ni mwendelezo wa ushirikiano huo."

Mbali na mambo mengine,maboresho hayo yataiwezesha tume kuwaondoa watu waliopoteza sifa ya kuandikishwa katika daftari hilo na hawana sifa za kupiga kura.

Aliyewekwa kizuizini kama mhalifu, ulemavu wa akili, kutiwa hatiani kwa kosa ambalo adhabu yake ni kifo au mtu anayetumikia adhabu zaidi ya miezi sita jela.
Tags
Daftari la Kudumu la Wapiga Kura
Habari
INEC Tanzania
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi
Watu wenye Ulemavu