Mahimbali aiagiza Tume ya Madini kuongeza kasi ya kutatua migogoro

DODOMA-Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Kheri Mahimbali ameiagiza Tume ya Madini chini ya Katibu Mtendaji wake, Mhandisi Yahya Samamba kuongeza kasi ya kutatua migogoro ya wachimbaji wa madini nchini.
Mahimbali ametoa maelekezo hayo leo Juni 27, 2024 alipotembelea Banda la Tume ya Madini katika Maonesho ya Wachimbaji Wadogo wa Madini Tanzania (FEMATA) yanayoendelea katika Viwanja vya Jakaya Convention Centre (JKCC) jijini Dodoma.
Amesema, Tume inafanya kazi nzuri ya kukusanya maduhuli, mapato yameongezeka na yanaonekana na kuitaka iongeze kasi ya kutatua changamoto za wachimbaji wadogo wa madini kwa kuwa wanachangia asilimia 40 ya mapato katika Sekta ya Madini

"Msi -ignore wachimbaji wadogo, STAMICO hata kama ni walezi na nyie Tume mna 'role' yenu, "amesema Mahimbali.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news