Mawaziri wa elimu EAC wakutana Dar

DAR-Mawaziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Utamaduni na Michezo kutoka Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) wamekutana Juni 22, 2024 jijini Dar es Salaam kushiriki Mkutano wa Kisekta wa 19 wa EAC.Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb.) ameshiriki mkutano huo na kubainisha kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesisitiza umuhimu wa matumizi ya lugha ya Kiswahili katika vikao vya sekta hiyo na vikao vya Jumuiya ya Afrika Mashariki na hatimaye waweze kuikuza na kuipeleka hoja kwa Mataifa.
"Pia tumejadili umuhimu wa kukuza elimu, sayansi, teknolojia, utamaduni na michezo kwa manuufaa ya sasa na mahususi kabisa kwa taasisi zetu kuangalia mitaala ambayo ipo katika masuala ya takwimu, sayansi, elimu na kiswahili kwa malengo ya kuboresha mitaala hiyo ili iwe bora zaidi na iweze kutumika na wanajumuiya ya Afrika Mashariki vizuri," amesema Waziri Ndumbaro.

Aidha, ameeleza kuwa wameongelea uwepo wa mashindano makubwa ya Afrika (AFCON) mwaka 2027 ambapo amesema wao kama Tanzania kwa kushirikiana na Kenya, Uganda watakuwa wenyeji kwenye mashindano hayo.
Mwisho amesema nchi zingine zote za jumuiya ya Afrika Mashariki wafahamu kwamba wao pia watakuwa wenyeji kwa namna moja ama nyingine kwenye mashindano hayo.

Kwa upande wake Waziri wa Jinsia, tamaduni, sana na torati za Taifa katika nchi ya Kenya, Mhe. Aisha Juma, amesema kwa mwaka huu wao ndio wanaandaa siku ya ulimwengu ya kiswahili ambayo itaadhimishwa Julai 7, 2024.

Amesema,maandalizi yako tayari ikiwemo kuwaalika wanajumuiya wote kwa ajili ya kusherehekea siku hiyo muhimu.

Ameeleza kuwa, Kiswahili ni lugha inayotumika sana ulimwenguni ambapo takribani watu milioni 500 wanazungumza lugha ya kiswahili pia inasaidia kukuza uchumi.
Ujumbe wa Tanzania katika Mkutano huu wa Mawaziri umeongozwa na Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb.) ambaye ameambatana na Naibu Waziri wa Elimu na Ufundi Stadi Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Ali Abdul - Gulam Hussein, Naibu Waiziri wa Elimu Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Omari Juma Kipanga, na Naibu Waziri Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) anayeshughulikia Elimu,Mhe. Zainabu Katimba (Mb.)

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news