Mkoa wa Kimadini Chunya wakusanya zaidi ya shilingi bilioni 30

●Kiasi cha gramu 8189.79 zakamatwa

●Leseni 65 za ununuzi mkubwa wa madini zatolewa

MBEYA-Mkoa wa kimadini Chunya mpaka kufikia Juni 7, 2024 umefanikiwa kukusanya maduhuli ya shilingi bilioni 34.9 katika mnyororo wa uchimbaji madini.
Hayo yamebainishwa leo Juni 7, 2024 na Afisa Madini Mkazi (RMO) mkoa wa kimadini Chunya, Mhandisi Laurent Mayala wakati akiwasilisha taarifa ya mwenendo wa sekta ya Madini wilayani Chunya kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Kheri Mahimbali.
Mhandisi Mayala amesema kuwa kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 Ofisi imefanikiwa kudhibiti matukio ya utorosha madini ambapo mpaka sasa kiasi cha gramu 8,189.79 za madini ya dhahabu zimekamatwa.

Akielezea kuhusu mwenendo wa utoaji leseni za ununuzi mdogo na mkubwa wa madini , Mhandisi Mayala amesema kuwa, idadi ya leseni 65 zimetolewa kwa wanunuzi wakubwa wa madini na leseni 315 za wanunuzi wadogo.
Akifafanua juu ya kuwaendeleza wachimbaji wadogo wilayani Chunya Mha.Mayala amesema kuwa tayari wametenga maeneo mbalimbali ikiwemo Makongolosi, Mawelo,Sagambi, Matundasi na Kasisi kwa ajili ya kurasimishwa kwa wachimbaji wadogo ili kukuza shughuli zao za uchimbaji.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Madini, Kheri Mahimbali ameipongeza Ofisi ya Madini Wilayani Chunya kwa kufanya vizuri katika usimamizi mzuri wa shughuli zote zinazohusiana na sekta ya madini.
Mahimbali ameongeza kuwa mkoa wa Kimadini Chunya ni mmoja wa mkoa muhimu sana katika sekta ya madini hivyo amewaataka watumishi kuendelea kufanya kazi kwa weledi , ushirikiano na kuongeza ubunifu ili kuendelea kufikia malengo yaliyowekwa.

Ziara hii ya siku mbili wilayani Chunya Mahimbali ameambatana na watendaji mbalimbali kutoka Wizara ya Madini kwa lengo la kukagua shughuli mbalimbali za uchimbaji , uzalisha na uchenjuaji katika mnyororo mzima wa sekta ya madini.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news