Kongamano kubwa la Madini Mkakati kufanyika Thailand, Watanzania kuongoza jopo kubwa duniani

BANGKOK-Asean Africa Minerals Investment Forum kwa kushirikiana na Tanzania-Thailand Chambers of Commerce chini ya uangalizi wa Consulate of Tanzania-Thailand wanaandaa kongamano la wadau mbalimbali wa madini mkakati (CRITICAL MINERALS) kuanzia Novemba 21 hadi 22,2024.
Ni madini ambayo yanahitajika katika kuendeleza viwanda ,uundaji wa magari ya umeme ikiwemo betri na vifaaa vya kielektroniki watakaokutana jijini Bangkok nchini Thailand.

Kongamano hilo linatoa fursa ya wadau wote kuhudhuria kwa kujisajili kupitia tovuti maalum ya kongamano ambayo ni https://aseanafricaminerals.org/
Pichani ni Mwenyekiti wa Asean Africa Minerals Investment Forum upande wa Afrika, ndugu Idrissa Songoro na kushoto ni Mwenyekiti wa Asean African Minerals Investment Forum upande wa Asean, ndugu Chiradej Sangthongsuk na katikati ni Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara wa Tanzania na Thailand na Balozi wa Heshima wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Thailand, Floreaan Rwehumbiza Laurean.Kwa pamoja wanaandaa kongamano hilo litalaowakutanisha wadau mbalimbali duniani Novemba 21 hadi Novemba 22,2024.

Pia, Watanzania watakaoshiriki na kuongoza jopo katika mjadala na mazungumzo ni Kamishna wa Madini mstaafu, Dkt.Dalay Peter Kafumu (Speaker), Mkurugenzi Mkuu mstaafu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazigira (NEMC), Dkt. Samuel Gwamaka (Panelist) na Godwin Martin Hiza Nyelo (Panelist).

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news