MWAUWASA yatunukiwa tuzo

DAR-Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mwanza (MWAUWASA) imetunukiwa tuzo kwa kuibuka mshindi wa pili miongoni mwa mamlaka za maji nchini katika utoaji wa taarifa kwa wananchi.
MWAUWASA imetunukiwa tuzo hiyo jijini Dar es Salaam Juni 21, 2024 na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Nape Nnauye (Mb) wakati wa kikao kazi cha Maafisa Habari Serikalini.
Tuzo hiyo imepokelewa na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma MWAUWASA, Mohamed Saif.

Aidha, mbali na tuzo hiyo, MWAUWASA imepokea Cheti cha kutambua jitihada za kipekee na mikakati bunifu ya mawasiliano inayotekeleza na ambayo imeleta mchango mkubwa katika Sekta ya Habari.
Kikao kazi hicho kimeshirikisha Maafisa Habari wa Serikali zaidi ya 500 kutoka Wizara, Taasisi, Mikoa na Halmashauri mbalimbali kote Nchini.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news