Rais Dkt.Mwinyi azindua Kigoda cha Taaluma cha Sheikh Abeid Amani Karume

ZANZIBAR-Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Mheshimiwa Dkt.Hussein Ali Mwinyi amekitaka Kigoda cha Taaluma cha Sheikh Abeid Amani Karume kutilia mkazo zaidi masuala ya kufanya tafiti mbalimbali kwa ajili ya maendeleo nchini.
Rais Dkt.Mwinyi ameyasema hayo Juni 15,2024 alipozindua rasmi Kigoda cha Taaluma cha Sheikh Abeid Amani Karume katika ukumbi wa Dkt.Ali Mohamed Shein uliopo Tunguu Mkoa wa Kusini Unguja.
Ameeleza kuwa, Serikali itafanya juhudi za kuhakikisha malengo ya kigoda hicho yanafanikiwa ili kuleta tija za kihistoria, kitaaluma na kimaendeleo kwa ustawi wa jamii.
Rais Dkt.Mwinyi amesema,kigoda hicho kiwe ni jukwaa ambalo litaendeleza na kutunza tunu za taifa za Mapinduzi na Muungano ambazo zimetimiza miaka 60.
Kwa upande mwingine Rais Dkt.Mwinyi amempongeza Profesa Egiland Pius Mihanjo kwa kuwa Mwenyekiti wa kwanza wa Kigoda hicho.

Viongozi mbalimbali wa Serikali,vyama vya siasa, vyombo vya ulinzi na usalama wameshiriki wakiwemo Rais mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete,
Marais wastaafu wa Zanzibar,Dkt. Amani Abeid Karume na Dkt.Ali Mohamed Shein na mwanasiasa mkongwe Mzee Stephen Wassira.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news