Rais Dkt.Samia awasili Afrika Kusini

PRETORIA-Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan amewasili nchini Afrika Kusini usiku wa leo Juni 18,2024 ambapo kesho Juni 19,2024  anatarajiwa kuhudhuria hafla ya uapisho wa Rais mteule wa nchi hiyo, Cyril Ramaphosa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa Ndege wa Waterkloof Pretoria nchini Afrika Kusini tarehe 18 Juni, 2024. Rais Samia anatarajia kuhudhuria hafla ya Uapisho wa Rais wa nchi hiyo Cyril Ramaphosa tarehe 19 Juni, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Watanzania waishio Afrika Kusini mara baada ya kuwasili Pretoria tarehe 18 Juni, 2024. Rais Samia anatarajia kuhudhuria hafla ya Uapisho wa Rais wa nchi hiyo Cyril Ramaphosa tarehe 19 Juni, 2024.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akifurahia jambo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Afrika Kusini,Dkt. Grace Naledi Pandor pamoja na Thembi Nkadimeng Waziri wa Utawala na Ushirika na Masuala ya Jadi. Rais Samia anatarajia kuhudhuria hafla ya Uapisho wa Rais wa nchi hiyo Cyril Ramaphosa tarehe 19 Juni, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akisaini Kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Waterkloof Pretoria nchini Afrika Kusini tarehe 18 Juni, 2024. Rais Samia anatarajia kuhudhuria hafla ya Uapisho wa Rais wa nchi hiyo Cyril Ramaphosa tarehe 19 Juni, 2024.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news