Shilingi milioni 12 za taka zampeleka jela miaka 20 Mtendaji wa Mtaa wa Oysterbay

DAR- Aliyekuwa Mtendaji wa Mtaa wa Oysterbay katika Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, Chema Hamis Kalembo amehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela bila faini, kwa ubadhirifu wa shilingi milioni 12 za makusanyo ya ada ya taka mtaani.

Hukumu hiyo imetolewa Juni 24, 2024 kupitia kesi ya Uhujumu Uchumi Na. 11/2022 mbele ya Mheshimiwa Isiaqa Kuppa, Hakimu Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni.

Katika shauri hilo lililoendeshwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi Janeth Kafuko, Mahakama imemtia hatiani mshtakiwa huyo kwa kosa la ubadhirifu kinyume na kifungu cha 28(1) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa [CAP 329 RE 2019].

Vikisomwa pamoja na Sheria ya Uhujumu uchumi Paragraph 21 ya Jedwali la kwanza na kifungu cha 57(1) na 60(2) cha Sheria ya Uhujumu Uchumi.
Ifahamike kuwa, mshtakiwa akiwa Afisa Mtendaji wa Serikali ya Mtaa wa Oysterbay alitenda kosa hilo la ubadhirifu wa fedha za umma kiasi cha shilingi 12,000,000.

Fedha ambazo zilikuwa ni za makusanyo ya ada ya taka alizotakiwa kuziwasilisha benki na badala yake kuzitumia kwa matumizi yake biafsi.

Mahakama imefikia uamuzi huo baada ya upande wa Jamhuri kuthibitisha kesi pasipo kuacha shaka yoyote.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news