Watanzania tuendelee kudumisha amani,upendo na mshikamano-Waziri Mkuu

DAR-Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametoa wito kwa Watanzania kuendelea kudumisha amani, upendo, umoja, mshikamano, kuhurumiana sambamba na kujiepusha na vitendo vinavyoashiria vurugu, uonevu na uvunjifu wa amani.
Pia amewasihi waimarishe malezi kuanzia ngazi ya familia ili kuepuka athari za mmomonyoko wa maadili nchini na kuhakikisha mienendo ya vijana na wanajamii wote inazingatia mila, desturi na tamaduni zetu.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo Jumatatu, Juni 17, 2024 wakati wa hafla ya Baraza la Idd El-Adh’haa Kitaifa lililofanyika katika Msikiti wa Mfalme Mohamed VI Bakwata Makao Makuu, Kinondoni jijini Dar es Salaam.
“Ninawashukuru nyinyi na madhehebu yote ya dini kwa kuendelea kuiombea nchi yetu amani, mshikamano na utulivu. Amani tuliyo nayo, ndiyo chachu kubwa ya kufikia mafanikio ya maendeleo ya kijamii, kisiasa na kiuchumi.”

Waziri Mkuu ametumia nafasi hiyo kuwapongeza BAKWATA kwa mipango na uratibu mzuri wa shughuli za ibada ya Hijja kwa mahujaji wa Tanzania kwa mafanikio makubwa na Serikali itaendelea kutoa ushirikiano wa dhati ili kuwezesha Waislamu kutekeleza nguzo hiyo muhimu. Pia ametoa wito kwa BAKWATA wasimamie weledi wa taasisi zote zinazowapeleka waislamu hija kama wanavyoratibu wao.
Awali, Katibu Mkuu wa BAKWATA, Alhaj Nuhu Jabiri Mruma amewasihi waislamu na Watanzania kwa ujumla waendelee kujenga umoja bila kujali madhehebu yao ili waendelee kuilinda na kudumisha amani kwani bila amani hawaweza kupata fursa ya kufanya ibada na shughuli zingine za kimaendeleo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news