DAR-Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametoa pongezi za dhati kwa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) kwa kupata safu mpya ya uongozi wa Rais, Makamu wa Rais na Katibu kwenye uchaguzi uliofanyika tarehe Juni 21, mwaka huu.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh6Hhk8I3x2rU5ZLPCV6uZNNa8l4gOTgpjOkAkVmEQx2IljPr0x4la1dw79-QIJj-ikn_sRUPgLZ2IuAlBVVYZ3vLW9X_hktutLMK-o6NbFI8Jv-K5lD4jbPdv40_ZaWjplL_7zjD5iwcaD59TLIJc4OBR8JNFwAMT0XWc7ln6BzMC7gHKZnM2mvBp9CF4/s16000/IMG-20240629-WA0067.jpg)
Viongozi waliochaguliwa katika uchaguzi huo ni Mhashamu Wolfgang Pisa Askofu wa Jimbo Katoliki la Lindi (Rais), Mhashamu Eusebius Nzigilwa Askofu wa Jimbo Katoliki la Mpanda (Makamu wa Rais) na Padre Charles Kitima Padre wa Jimbo Katoliki la Singida (Katibu Mkuu).
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi7smaQQR8Dm_fevGjqOkYRQm0NOcoL-jxS7v70a9KT_9__qPK5WnH0HbCHd86UKReffDRH8FvVQMYw7C0hriQm17-7NoAW_TP5w1Sc_KYQ5UZhRptESTvnUeH_hrPLfLW973W6KZGRxiKwClOY3STu3RAvIzdL5RptzAAVUxj6GnXGXg9zcQ4UgTf1T_w/s16000/IMG-20240629-WA0066.jpg)
“Mungu awabariki viongozi wote na kuwasimamia katika majukumu yenu,” amesema Waziri Mkuu.