Alex Msama atunukiwa Tuzo ya Heshima

DAR-Mbobezi wa kukuza nyimbo za injili, msambazaji na muandaaji wa matamasha ya injili Tanzania ambaye pia ni Mkurugenzi wa Msama Promotions, Mheshimiwa Alex Msama jana Julai 20, 2024 jijini Dar es Salaam ametunukiwa Tuzo ya Heshima.
Msama ametunukiwa tuzo hiyo ya heshima na Clouds Media Group, kwa kutambua mchango wake mkubwa kwa kuwa mwanzilishi wa kipindi cha Gospel cha Clouds FM.
Mkurugenzi wa Msama Promotions, Alex Msama akiitazama tuzo yake ya heshima.
Mkurugenzi wa Msama Promotions, Alex Msama akipokea tuzo ya heshima kutoka Clouds Media Group, kwa kutambua mchango wake mkubwa kwa kuwa mwanzilishi wa kipindi cha Gospel cha Clouds FM.

Mbali na haho, ikumbukwe kuwa, Alex Msama amekuwa na mchango mkubwa katika kuufanya muziki wa injili kuendelea kufahamika na kupendwa zaidi ndani na nje ya Tanzania.

Licha ya kufahamika waimbaji wengi wameweza kuitumia fursa hiyo kujipatia vipato na kuziendea ndoto zao, kwani licha ya Msama kuupromoti muziki huo amekuwa msambazaji wa kazi hizo za injili huku akiandaa matamasha ya Kimataifa hapa nchini kila mwaka.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news