Balozi Kasike, TIC waweka mikakati kuzifikia fursa Msumbiji

DAR-Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Msumbiji,Mheshimiwa Phaustine Kasike amekutana na Bw. John Mathew Mbali, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC).
Mkutano huo umefanyika kwenye ofisi za TIC zilizopo Posta jijini Dar es Salaam ambapo viongozi hao wamejadiliana kuhusu kufanya kazi kwa ukaribu ili kuwafikia wadau wa biashara na uwekezaji kutoka Msumbiji ili kuja kuwekeza Tanzania.

Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Msumbiji.

Aidha, viongozi hao wamekubaliana kuanzia sasa kuzishawishi mamlaka na wadau wengine wa biashara na uwekezaji kutoka Tanzania na Msumbiji kushiriki katika matukio mbalimbali ya kibiashara yanayofanyika katika nchi hizi ili kupata fursa ya kutangaza bidhaa na huduma wanazotoa kwa lengo la kupata masoko.
Kwa upande wake, Mhe. Balozi Kasike ameeleza kwamba katika Utekelezaji wa Sera ya Diplomasia ya Uchumi, moja ya Jukumu la Msingi la Ubalozi ni kuziunganisha taasisi na wadau wengine wa Sekta ya Biashara na Uwekezaji kutoka Tanzania.

Pia,kufanya kazi kwa ukaribu na wenzao wa Msumbiji kwa maslahi ya nchi zetu mbili. Hivyo, aliahidi kutoa kila aina ya ushirikiano katika kutekeleza jukumu hilo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news