MTWARA-Msafara wa Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi leo Julai 28,2024 akiwa njiani kuelekea Mtwara Mjini baada ya kuzungumza na Wananchi na Wanachama wa Masasi amesimamishwa na wananchi katika eneo la Kata ya Nganganga Jimbo la Ndanda wakitaka awasalimie na kuzungumza nao.

Katibu Mkuu wa CCM na Wajumbe wa Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, anaendelea na ziara ya mikoa miwili inayolenga kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2020/2025, kukagua na kuhamasisha uhai wa CCM kuanzia ngazi ya shina, pamoja na kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia majawabu.