Balozi Yakubu aongoza maafisa Ubalozi kutembelea kiwanda cha mfanyabiashara mwenye asili ya Tanzania nchini Comoro

MORONI-Maafisa wa Ubalozi wa Tanzania nchini Comoro wakiongozwa na Balozi wa Tanzania nchini humo,Saidi Yakubu tarehe 17,2024 wametembelea kiwanda cha maji cha Aden kinachomilikiwa na Mfanyabiashara mwenye asili ya Tanzania, Khalil Bakhressa.
Bw.Bakhressa aliueleza ujumbe huo kuwa hivi sasa wanazalisha maji hayo kwa wingi zaidi na wako mbioni kuanzisha kiwanda cha maziwa na bidhaa zitokanazo na maziwa kwa kushirikiana na kampuni za Tanzania.
Kiwanda cha Aden ni miongoni mwa viwanda vikubwa vya maji nchini Comoro.
Kwa upande wake Balozi Yakubu alimpongeza Bwana Bakhressa kwa maendeleo ya kiwanda chake ikiwa ni kielelezo cha mafanikio ya watanzania diaspora na kumuahidi ushirikiano pale inapohitajika.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news