Barabara ya Tabora hadi Mpanda unateleza na lami tu-Rais Dkt.Samia

KATAVI-Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ameeleza kuwa Serikali inaendelea kuboresha miundombinu ya barabara katika Mkoa wa Katavi ambapo sasa barabara ya kutoka Tabora hadi Mpanda (km 352) ni ya kiwango cha lami.
Rais Dkt. Samia ameeleza hayo leo Julai 13, 2024 wakati akizungumza na wananchi wa Inyonga Wilayani Mlele wakati wa ziara yake mkoani Katavi.
“Wakati nimekuja kipindi cha kampeni kutoka Tabora kwenda Mpanda ilikuwa ni vumbi tupu lakini leo nimeteleza mpaka nimesinzia, Barabara ni nzuri na ni maendeleo makubwa sana, niwapongeze sana,"amesema Dkt. Samia.

Dkt. Samia ameeleza miradi mingine inayoendelea kutekelezwa na Serikali katika Mkoa wa Katavi ni pamoja na ujenzi wa barabara ya Kibaoni - Makutano ya Mlele (km 50), Vikonge - Luhafwe (km 25), Luhafwe - Mishamo (km 37) na Kagwira - Karema (km 110) kwa kiwango cha lami.
Aidha, Dkt. Samia ameeleza kuwa pamoja na miradi inayoendelea kutekelezwa, Serikali ipo katika hatua za kutafuta Makandarasi wa kutekeleza miradi mingine ya miundombinu ya barabara katika Mkoa wa Katavi.

Ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Katavi kutunza na kulinda miundombunu ya Barabara iliyokamilika na inayoendelea kutekelezwa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news