DAR-Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Emmanuel Tutuba, ametembelea banda la BoT kwenye Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yanayofanyika katika viwanja vya Julius Nyerere Barabara ya Kilwa, Temeke, jijini Dar es Salaam.


Pia, BoT inatoa elimu kuhusu utambuzi wa alama za usalama katika noti za Tanzania na njia sahihi za utunzaji wa noti na sarafu. Wananchi wanaotembelea banda la BoT wanapata fursa ya kuona na kujifunza kwa vitendo alama hizi muhimu zinazosaidia kutambua noti halali za Tanzania.

Jitihada hizo za BoT zinachangia kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu masuala ya kifedha na kuwajengea uwezo wa kufanya maamuzi sahihi ya kifedha, hivyo kuchangia kwa kiasi kikubwa katika kukuza sekta ya fedha na uchumi wa nchi kwa ujumla.