BoT yatoa elimu ya utambuzi wa alama za usalama katika noti na utunzaji kwa kundi maalum la wasioona Dodoma

DODOMA-Benki Kuu ya Tanzania imeendesha semina kuhusu utambuzi wa alama za usalama katika noti pamoja na namna sahihi ya utunzaji wa noti na sarafu kwa kundi maalum la wasioona jijini Dodoma.
Katika semina hiyo, washiriki walielimishwa jinsi ya kutambua noti halali kwa kutumia alama maalum za usalama ambazo zinaweza kuguswa au kuhisiwa kwa mikono.
Pia, walipata mafunzo kuhusu njia bora za kutunza noti na sarafu ili kuhakikisha zinadumu kwa muda mrefu na kusaidia kupunguza gharama za kuchapisha noti mpya kufidia zilizoharibika.
Lengo la semina hiyo ni kuhakikisha wasioona wanapata elimu itakayowawezesha kushiriki kikamilifu katika shughuli za kifedha na kiuchumi kwa usalama na ufanisi zaidi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news