DAR-Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Emmanuel Tutuba,tarehe 23 Julai, 2024 amekutana na Balozi wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri nchini Tanzania, Mhe. Sherif Ismail, na kujadiliana masuala mbalimbali ya kuimarisha ushirikiano katika sekta ya fedha na uchumi kiujumla.
Akizungumza katika mkutano huo, Gavana Tutuba amesema Benki Kuu ya Tanzania itaendelea kuimarisha ushirikiano uliopo kati yake na Benki Kuu ya Misri pamoja na Serikali ya nchi hiyo kupitia programu mbalimbali za kukuza uchumi baina ya nchi hizo.




Kwa upande wake, Balozi Sheriff Ismail, ameipongeza Benki Kuu kwa mchango wake katika kusimamia uchumi wa nchi na ameahidi kuendelea kushirikiana na Serikali katika kutekeleza programu mbalimbali zenye manufaa ya kiuchumi kwa nchi zote mbili.