Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo Julai 5,2024

SONGWE-Mfamasia wa Kituo cha Afya cha Isansa kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi mkoani Songwe, Daudi Kwibuja (30) amefariki kifo cha kutatanisha na mwili wake kukutwa kando ya barabara kuu itokayo Mbeya kwenda Tunduma katika eneo la Mlowo wilayani humo.
Mwili wa mtumishi huyo wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi katika Idara ya Afya umekutwa ukiwa na majereha mwilini mwake na tayari Jeshi la Polisi limeanzisha uchunguzi.
Akitoa taarifa ya kifo hicho, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, Agostino Senga amesema kuwa, uchunguzi unaonesha mtumishi huyo aliuawa usiku wa Julai 3, 2024 na mwili wake kukutwa ukiwa umetupwa kando ya barabara hiyo Julai 4, 2024, majira ya asubuhi.

Kamanda Senga amesema, licha ya kuwa awali kudhaniwa kuwa marehemu alifariki kwa ajali ya kugongwa na gari, lakini baada ya mwili huo kuchunguzwa umekutwa na majeraha ambayo hayafanani na ya ajali ya kugongwa na gari.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news