HAZINA TV:Refa Msaidizi wa Video (V.A.R) rasmi Benjamin Mkapa Stadium

DAR-"Nimetembelea banda la Wizara ya Fedha, Wizara ya Fedha yenyewe pamoja na taasisi zake nyingi zipo ndani ya banda hili, kwa wananchi niwaambie maonesho ni mazuri sana, yana mambo mengi muhimu ukitaka elimu, ikiwemo elimu ya kodi, elimu ya fedha na kwa namna gani Serikali inafanya kazi, karibu Sabasaba.

"Katika banda la Wizara ya Fedha nimefurahi kutembelea kitengo cha kodi, moja mnatoa elimu ya kodi na tunajua kodi ni muhimu sana katika uchumi wa nchi yetu.
"Katika elimu ya kodi nimetembelea na nimejifunza ni kwa namna gani misamaha ya kodi huwa inatolewa. 

"Miongoni mwa wanufaika wakubwa wa misamaha ya kodi ni wadau wote wa michezo ambao kupitia sheria iliyotungwa ya mwaka huu, tumepata msamaha wa baadhi ya vifaa vya michezo na kwa kuanzia mtambo wa VAR ambao umefungwa katika Uwanja wa Benjamin Mkapa,...tayari umeshafungwa na tayari watu wameshapewa mafunzo, Serikali imesamehe kodi ya mtambo ule ili wapenda michezo waweze kunufaika,"amesisitiza Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mheshimiwa Dkt.Damas Ndumbaro katika mahojiano na Hazina TV.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news