Jaji Mkuu asifu Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kutafsiri sheria kutoka Kiingereza kwenda Kiswahili

DAR-Jaji Mkuu wa Tanzania,Mhe. Prof Ibrahim Hamis Juma tarehe 5 Julai,2024 ametembelea banda la Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali lililoko kwenye Maonesho ya Sabasaba jijini Dar es Salaam.
Akiwa bandani hapo, Mhe. Jaji Mkuu alisifu jitihada za Ofisi ya Mwanasheria Mkuu za kuamua kutafsiri sheria mbalimbali na kuwa lugha ya Kiswahili huku akitaka ufafanuzi kama baada ya tafsiri sheria zitakuwa zinapatikana kwa lugha ya Kiswahili na Kiingereza.

"Niwapongeze kwa kutafsiri sheria kutoka Kiingereza kuwa Kiswahili, zitakuwa zinapatikana kwa lugha ya kiswahili na kingereza?."

Akitoa maelezo kwa Mhe Jaji Mkuu wa Tanzania, Wakili Mwandamizi wa Serikali kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Bi. Angella Kimaro amesema sheria hizo zitapatikana kwa lugha ya Kiswahili na kingereza.

"Sheria hizi Mhe. Jaji zitapatikana kwa lugha zote mbili kupitia mifumo yetu, pia katika wananchi watapa kuziona sheria zilizofanyiwa marekebisho kupitia madirisha yaliyoko kwenye mifumo yetu,"asema Bi.Angella.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news