Jikiteni katika utoaji elimu

DAR-Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Jaji Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi, amesisitiza utoaji wa elimu kuhusu masuala mbalimbali ya kisheria kwa wananchi.
Mhe. Jaji amesema hayo Julai 5,2024 alipotembelea banda la Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali lililoko kwenye maonesho ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam.
"Endeleeni kutoka elimu kwa wananachi, hakikisheni wananchi wengi wanapata uelewa wa masuala haya kisheria, mshirikiane na Wizara ya Katiba na Sheria katika kutoa huduma ya msaada wa kisheria kupitia kampeni ya msaada wa Kisheria ya Mama samia ili muweze kuwafikia watu wengi zaidi," amesema Mhe. Feleshi.

Akipokea maelekezo ya Mhe. Feleshi, Wakili Mwandamizi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bi. Angella Kimaro ameeleza mwenendo wa ushiriki wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika maoenesho hayo, ambapo amesema wananchi wamekuwa wakija kupata ushauri na wengi wao wakiwa wanataka kufahamu majukumu ya hiyo.
"Tumepokea maelekezo yako Mhe. Jaji, pia katika banda letu tunapata wananchi ambao wanakuja kupata ushauri wa kisheria pamoja kufahamu kuhusu majukumu ya ofisi yetu," alisema. Bi angella.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news