JMAT waipa kongole Ofisi ya Waziri Mkuu maonesho ya 48 ya Sabasaba

DAR-Viongozi wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT) wameipongeza Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na Taasisi zake kwa kuendelea kuelimisha na kuhabarisha wananchi na wadau juu ya masuala mbalimbali yanayotekelezwa na ofisi hiyo ikiwemo masuala ya Kazi, Maendeleo ya Vijana, Ajira na Ukuzaji Ujuzi.
Pamoja na Menejimenti ya Maafa, Uratibu wa shughuli za Serikali na fursa za uwezeshaji wananchi kiuchumi.
Pongezi hizo zimetolewa leo Julai 13, 2024 wakati walipotembelea banda jumuishi la Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na taasisi zake katika maonesho ya 48 ya biashara ya kimataifa (Sabasaba) jijini Dar es salaam.

Aidha, viongozi hao wametembezwa na kujionea huduma mbalimbali zinazotolewa na ofisi hiyo.
Maonesho hayo yamefungwa rasmi leo Julai 13, 2024 na Mheshimiwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussen Mwinyi ambapo yalikuwa yakiongozwa na kauli mbiu isemayo "Tanzania: Mahali Sahihi Pa Biashara na Uwekezaji,"

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news