Joe Biden ajiondoa kugombea urais Marekani

WASHINGTON DC-Rais wa Marekani,Joe Bide ametangaza kujiondoa kwenye kinyang’anyiro cha ugombea Urais wa nchi hiyo.
Ni katika uchaguzi ujao akisema anafanya hivyo kwa maslahi mapana ya chama chake na Taifa la Marekani kwa ujumla, Biden anachukua uamuzi huo ikiwa imebaki miezi minne tu kwa Marekani kufanya uchaguzi wa Urais.

Aidha,uamuzi wa Biden umekuja huku kukiwa na mpasuko ndani ya chama chake wengine wakiamini angeweza kugombea tena na wengine wakisema hatoweza.

Ni kutokana na uzee na kuzidiwa hoja wakati wa mdahalo wake na mpinzani wake Donald Trump ambaye hivi karibuni alinusurika kuuawa kwa risasi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news