Magazeti leo Julai 14,2024

MWANZA-Jeshi la Polisi mkoani Mwanza linawasaka wananchi waliozusha taarifa za kupigwa hadi kufariki mwanafunzi wa kidato cha pili katika Shule ya Sekondari Mlimani iliyopo Kata ya Bugarika wilayani Nyamagana, Leonia Amiri (16).
Uzushi huo ulitokea Julai 11,2024 ikidaiwa mwanafunzi huyo alipigwa na mwalimu hadi kumsababishia kifo, hatua iliyopelekea wananchi kukusanyika shuleni hapo kwa fujo, akiwemo mama mzazi wa mwanafunzi, Christina Joshua (35) ambaye tayari anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Mwanza.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Naibu Kamishna wa Polisi, DCP Wilbrod Mutafungwa ametembelea kata hiyo kuwapatia wananchi elimu ya ulinzi na usalama huku akiwataka kuifanyia uchunguzi taarifa yoyote wanayopokea, badala ya kufanya uzushi unaoweza kupelekea uvunjifu wa amani katika jamii.





Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news