Magazeti leo Julai 20,2024

DODOMA-Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imeongeza kasi ya kushughulikia malalamiko ya uvunjwaji wa haki za binadamu na misingi ya utawala bora.

Ni kutokana na upatikanaji wa rasilimali fedha kwa ajili ya uchunguzi ambapo kwa mwaka 2022/23 tume hiyo ilikuwa ikishughulikia jumla ya malalamiko 1,524 ambapo ilihitimisha jumla ya malalamiko 789 na kufanya malalamiko yaliyoendelea kuanzia Julai 1, 2023 kuwa 885.
Hayo yamebainishwa Julai 19,2024 jijini Dodoma na Mwenyekiti wa tume hiyo, Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ripoti mbalimbali za chunguzi zilizofanywa na tume kwa Mwaka wa 2023/24.
Pia, amesema katika kipindi cha kuanzia Julai 10,2023 hadi Mei 30,2024 THBUB ilipokea malalamiko mapya 135 na kufanya malalamiko yanayoshughulikuwa mwaka huo kuwa malalamiko 1,020 ambapo katika katika kipindi husika THBUB ilifanikiwa kukamilisha na kuhitimisha uchunguzi wa malalamiko 236 na hivyo uchunguzi malalamiko 784 unaendelea.
Mwenyekiti huyo ameongeza kuwa, katika malalamiko hayo, malalamiko 22 yaliilazimu THBUB kufanya uchunguzi maalum huku chunguzi hizo zikihusu masuala ya ardhi, uharibifu wa mazingira, tuhuma za vitendo vya ukatili katika vizuizi na matumizi mabaya ya madaraka.


Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news