Magazeti leo Julai 21,2024

KIAMBU-Wizara ya Afya nchini Kenya imetoa tahadhari baada ya trela lililobeba sumu kali aina ya Sodium Cyanide kuanguka katika eneo la Kambembe huko Rironi katika Kaunti ya Kiambu.Sodium Cyanide inatajwa kuwa mojawapo ya sumu kali zaidi duniani, kutokana na uwezo wake wa kusababisha kifo mara moja. 

Ina rangi nyeupe, na huweza kuchanganyika kwa wepesi na maji na vyuma pia, jambo linaloifanya kuwa hatari.
Kwa mujibu wa Taifa Leo, taarifa kutoka kwa Katibu wa wizara hiyo,Mary Muthoni inasema kwamba umma unatahadharishwa dhidi ya kusogelea eneo hilo la mkasa, kwa sababu kemikali hiyo ni hatari mno kiasi cha kusababisha kifo iwapo mhusika anatagusana nayo kwa wingi.
Ni madini ambayo yanatumika katika uchimbaji dhahabu, kutokana na uwezo wake wa kuyeyusha dhahabu kwa umakinifu mkubwa, kutoka kwa tope au mchanganyiko mwingine, katika shughuli inayofahamika kisayansi kama Cyanidation.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news