Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) yakusanya shilingi trilioni 27.64

DAR-"Kwa niaba ya Bodi ya Wakurugenzi, Menejimenti ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inapenda kuufahamisha umma kuwa katika kipindi cha Mwaka wa Fedha 2023/24, imefanikiwa kukusanya kiasi cha Shilingi Trilioni 27.64, ambayo ni sawa na ufanisi wa asilimia 97.67 ya lengo la kukusanya Shilingi Trilioni 28.30.

"Makusanyo haya ni ongezeko la asilimia 14.50 ikilinganishwa na makusanyo ya Shilingi Trilioni 24.14 katika Mwaka wa Fedha uliopita, 2022/23.

"Katika kipindi cha robo mwaka ya nne yaani Aprili - Juni, 2024, TRA imefanikiwa kukusanya kiasi cha Shilingi Trilioni 7.09, sawa na ufanisi wa asilimia 99.46 ya lengo la kukusanya kiasi cha Shilingi Trilioni 7.13.

"Makusanyo haya ni ongezeko la asilimia 24 ukilinganisha na kiasi cha Shilingi Trilioni 5.72 kilichokusanywa katika kipindi kama hicho kwa Mwaka wa Fedha uliopita 2022/23;

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news