DODOMA-Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Jumanne Sagini ameipongeza Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kuendelea kushirikiana na Wizara ya Katiba na Sheria katika utatuzi wa changamoto mbalimbali pamoja na kutoa huduma bora za kisheria kwa wananchi na Serikali kwa ujumla.


“Lengo letu ni Sekta yetu kuweza kupata mahitaji yatakayoweza kusaidia kufanikisha majukumu muhimu kwa wananchi na Serikali katika ubora na ufanisi mkubwa.”

Awali, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Balozi Prof. Kennedy Gastorn akisoma taarifa fupi kwa Mhe. Naibu Waziri alitaja baadhi ya mafanikio yaliyopatikana ni pamoja na jumla ya sheria 300 zimefanyiwa tafsiri kwa lugha ya Kiswahili ,huku sheria hizo zikisubiriwa kutangazwa katika toleo la Urekebu la mwaka 2023.
Akifafanua zaidi, Mhe. Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali ametaja mambo kadhaa ambayo, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imefanikisha kuandaa hadi sasa kuwa ni pamoja na maazimio kumi ya kuridhia mikataba na itifaki mbalimbali yaliyoandaliwa na kuwasilishwa katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.