Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha atembelea banda la PPAA maonesho ya Sabasaba

DAR-Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bw. Elijah Mwandumbya ametembelea banda ya Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) katika Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yanayoendelea jijini Dar es Salaam.
Pamoja na mambo mengine, Bw. Mwandumbya alifahamishwa na watumishi wa PPAA kuhusu majukumu ya PPAA ikiwa ni pamoja na kuanzishwa kwa moduli mpya ya uwasilishaji wa malalamiko/rufaa kwa njia ya kieletroniki.
Naibu Katibu Mkuu alitembelea banda la PPAA hivi karibuni alipofanya ziara ya kujionea Maonesho ya Sabasaba yaliyoanza 28 Juni - 13 Julai, 2024.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news