Naibu Waziri Sillo aongoza kikao cha dharura cha Baraza la Usalama la Taifa Barabarani

DAR-Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Daniel Sillo (Mb) ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani nchini, ameongoza Kikao cha Dharura Na.1/2024 cha Baraza hilo kilichofanyika leo Julai 18, 2024 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi Ndogo za Wizara hiyo jijini Dar es Salaam.
Kikao hicho kimejadili agenda mbalimbali ikiwemo Mikakati na Maandalizi katika kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani kwa Mwaka 2024 na Miaka 50 ya Baraza hilo ambayo Kitaifa yanatarajiwa kufanyika mkoani Dodoma.
Awali akisoma taarifa yake Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani ambaye ni Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Kamishna Msaidizi wa Polisi Ramadhan Ng’anzi ameeleza kuwa Hali ya Usalama Barabarani nchini imeendelea kuimarika kutokana na utekelezaji wa Operesheni za ukamataji wa makosa hatarishi, Utoaji wa elimu, Ukaguzi wa magari na usimamizi wa watendaji wa Kikosi cha Usalama Barabarani.
Aidha, Wajumbe wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani walipata fursa ya kutoa maoni yao mbalimbali kuhusu agenda zilizojadiliwa katika Kikao hicho sambamba na kutoa ushauri wa nini kifanyike katika kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani kwa Mwaka 2024 na Miaka 50 ya Baraza hilo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news