NSSF yawataka watumishi wanaotarajiwa kustaafu kuanza kujiandaa mapema

DAR-Mfuko wa Taifa wa Hifadhi za Jamii (NSSF) umewataka watumishi wanaotarajiwa kustaafu kuanza kujiandaa ikiwa ni pamoja na kuhakiki taarifa zao za msingi.
Sambamba na kuwa na nidhamu ya matumizi ya fedha,hali itakayosaidia kupunguza changamoto za maisha pindi wanapostaafu.

Rai hiyo imetolewa na Meneja wa Mafao wa NSSF Ilala, Mrisho Mwisimba wakati akimuwakilisha Mkurugenzi wa Uendeshaji NSSF katika warsha iliyolenga kutoa elimu kwa watumishi wanaotarajia kustaafu.
Ni kutoka katika Mkoa wa Temeke ambapo pia amewasisitiza kuanzisha miradi salama ya uwekezaji ili kuwa na uhakika wa kipato endelevu.

Kwa upande wake Emmanuel Nyange ambaye ni Meneja Idara ya Biashara wa Benki ya Biashara ya Taifa (TCB), ambao pia walihudhuria mafunzo hayo kwa ajili ya kutoa elimu ya fedha katika mafao amesema kuwa, TCB imeamua kusimama na wastaafu kwa miaka 10 sasa ikijikita katika kutatua changamoto wanazokutana nazo wastaafu.

Ni kwa kuanzisha akaunti maalumu ya Kivulini isiyo na makato yeyote wala gharama za uendeshaji,lengo likiwa ni kumnusuru mstaafu
Nyange ameongeza kuwa, sambamba na hayo TCB imeanzisha huduma za pensheni advance inayomuwezesha mstaafu kupata fedha ya kujikimu kwa kutoa suluhu kwa tatizo analokutuna nalo,ila pia kuna huduma ya mkopo usio na masharti yoyote.

Aidha,kwa wastaafu watarajiwa TCB wanatoa huduma za fixed akaunti huku asilimia yake ikiwa ni mpaka 11 kwa mwaka, kupitia akaunti ya kivulini bado wastaafu wakipata majanga au ulemavu wa kudumu wanapewa fidia,na sababu kuu ni azimio la serikali kuweza kufikia makundi yote katika huduma za ujumuishaji wa kifedha.
Huduma hizo zote zinatolewa katika mukitadha wa kutatua changamoto wanazopitia wastaafu, hivyo kuwasihi wastaafu watarajiwa kuhakikisha wanasamehe na kuachana na yaliyopita na zaidi wafungue akaunti na TCB ili waweze kupata huduma zote hizo.

Kwa upande wake Afisa Mafao Mkuu wa NSSF, Shakira Masoli amewasisitiza watumishi kujiandaa kustaafu kwa kuhakikisha wanapeleka na wanahakiki taarifa zote za msingi ili kuepusha usumbufu pindi wanapostaafu.
Naye mmoja wa wanufaika wa NSSF,Damas Nungu ameutaka mfuko huo kupunguza kikokotoo cha awali anachopewa mstaafu huku akiwahimiza waajiri kupeleka michango ya watumishi wao kwa wakati.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news