Rais Dkt.Mwinyi atembelea banda la Benki Kuu katika Maonesho ya Sabasaba

DAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametembelea banda la Benki Kuu ya Tanzania kwenye Maonesho ya Sabasaba jijini Dar es Salaam na kupokelewa na Gavana, Bw. Emmanuel Tutuba.
Katika ziara hiyo, Dkt Mwinyi amepewa maelezo kuhusu elimu inayotolewa kwa wananchi kuhusu kazi za Benki Kuu ikiwemo sera za fedha, namna ya kuwekeza katika dhamana za serikali, mifumo ya malipo ya taifa, na namna BoT inavyosimamia sekta ya fedha nchini.
Vilevile, Gavana Tutuba ameeleza kuhusu kazi za kitengo cha kupambana na utakasishaji fedha haramu na kazi zinazofanywa na Bodi ya Bima ya Amana.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news