Rais Dkt.Samia aahidi kufanya Royal Tour kuitangaza Hifadhi ya Katavi

KATAVI-Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameahidi kufanya filamu nyingine ya Royal Tour katika Hifadhi ya Taifa ya Katavi baada ya kujionea wanyamapori mbalimbali katika Hifadhi hiyo.
Dkt. Samia ameyasema hayo leo Julai 15, 2024 alipokuwa akizungumza na wananchi katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe mkoani Katavi.Kauli hiyo inafuatia ombi la Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Mizengo Pinda la kuomba Royal Tour nyingine ifanyike mkoani humo.
“Nataka nikiri kwamba zile sifa alizozisema Waziri Mkuu Mstaafu kuhusu uwepo wa wanyama wengi na wa kuvutia katika Hifadhi ya Katavi nimeziona mwenyewe na zimetimia maana leo nilipita kwenye mbuga hiyo kuona ikoje mahitaji yakoje.

“Tumeona mambo mengi ya kufanya mle ndani na suala la Royal Tour Waziri wa Maliasili na Utalii ameshaandika hivyo jipange na ukiwa tayari mimi mwenyewe nitakuja."
Rais Samia yupo katika ziara mkoani Katavi pamoja na mambo mengine kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani humo na leo ameingia mkoani Rukwa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news