Rais Dkt.Samia atengua uteuzi wa Waziri Nape Nnauye, January Makamba na Byabato

NA GODFREY NNKO

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametengua uteuzi wa mawaziri wawili na naibu waziri mmoja.
Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Julai 21,2024 na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka.

ZINAZOHUSIANA

Mawaziri waliotenguliwa ni Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari,Mhe. Nape Moses Nnauye (Mb.) ambaye nafasi yake imechukuliwa na Mhe. Jerry William Silaa (Mb.).

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa January Yusuf Makamba ambaye nafasi yake imechukuliwa na Balozi Mahmoud Thabit Kombo.

Balozi Kombo ameteuliwa kuwa Mbunge na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Kabla ya uteuzi huu Balozi Kombo alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Italy.

ZINAZOHUSIANA

Vile vile, Mheshimiwa Rais Dkt.Samia ametengua uteuzi aa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki,Mhe.Stephen Lujwahuka Byabato (Mb.) nafasi yake inachukuliwa na Mhe. Dennis Lazaro Londo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news