Rais Dkt.Samia awapongeza wakulima kwa utoshelevu wa chakula nchini

KATAVI-Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan amewapongeza wakulima kote Tanzania kwa kiwango cha uzalishaji wa chakula na kuifanya nchi kuwa na utoshelevu wa chakula unaozidi asilimia 120.
Ametoa pongezi hizo leo Julai 13,2024 wakati akihutubia katika kilele cha Wiki ya Wazazi pamoja na mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Azimio, Mpanda Mjini.Rais Dkt. Samia amesema,utoshelevu huo umesaidia nchi kudhibiti mfumuko wa bei ambao umebaki asilimia tatu na hivyo kuwaepusha wananchi na ugumu wa maisha unaotokana na uhaba wa chakula na mfumuko wa bei.
Vile vile, Rais Dkt. Samia amezitaka halmashauri zote katika Mkoa wa Katavi kuacha tabia ya kuwatoza wananchi ushuru wa mazao kwa kiasi kisichozidi tani moja na kufuata maelekezo yaliyotolewa na Serikali hapo awali.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news