RC Babu atangaza Maonesho ya Nanenane Kanda ya Kaskazini, asema yatakuwa ya mfano

NA ABEL PAUL

KAIMU Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Nurdin Babu ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ametangaza ufunguzi wa maonesho ya Nanenane Kanda ya Kaskazini ambapo amesema maonyesho hayo yataanza Agosti 01,2024 na kufunguliwa rasmi Agosti 03,2024.
Akitoa taarifa hiyo leo Julai 19,2024 jijini Arusha amesema maonyesho hayo ya thelathini maandalizi yake yameshaanza huku akiwaomba wananchi kujisajili na kulipia ada ya maonyesho hayo ambayo yamebeba kauli mbiu isemayeo chagua viongozi bora wa serkali za mitaa kwa maendeleo endelevu ya kilimo na mifugo.

Aidha, RC Babu amesema kuwa serkali ya Mikoa hiyo ya Kanda ya kaskazini inawaomba wananchi kuendelea kujisajili huku akiwaomba kuzingatia maelekezo kama yalivyoainishwa katika fomu iliyopo katika mtandao wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha ambapo amesema kuwa maonesho ya mwaka huu yatakuwa ya kipeke kuliko miaka mingine.

Sambamba na hilo ametumia fursa hiyo kuzikaribisha taasisi za kitaifa na kimaitaifa huku akiwataka kuwasilisha maombi yao mapema kuondoa usumbufu katika siku za mwisho Pamoja na wafanyabiashara wadogo wadogo kutoka kanda hiyo.

Pia amewaarika wananchi wote wa kanda ya kaskazini na wale wa mikoa mingine kufika Mkoani Arusha katika maonesho hayo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news