MANYARA-Mahusiano mazuri yaliyowekwa na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan yameendelea kuonekana kwa vitendo.

Mhe. Sillo amesema nchi itaendelea kudumisha amani na utulivu uliopo ili wawekezaji na wafadhili mbalimbali wafanye kazi zao bila hofu, hivyo amempongeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuifungua nchi, kuwavutia wawekezaji, kudumisha ulinzi na usalama na kutekeleza miradi ya maendeleo katika sekta zote.
"Nchi kama haipo salama huwezi kupata wafadhili kama hawa na kuwekeza pesa nyingi kiasi hiki."
Aidha,Mhe. Sillo amewaomba wakazi wa maeneo hayo ambayo yupo Mfadhili huyo waendelee kuboresha mahusiano mazuri yaliyopo ili aendelee kuwepo pia kuendelea kutunza miradi yote ambayo imeletwa katika maeneo yao.