Serikali yasisitiza matumizi ya takwimu sahihi kwa maendeleo

NA PETER HAULE

KAMISAA Sensa na Spika mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Anne Semamba Makinda, ametoa rai kwa wananchi kuanzia ngazi ya chini kutumia takwimu sahihi zilizopatikana kutokana na Sensa iliyofanyika katika shughuli mbalimbali za maendeleo.
Kamisaa wa Sensa na Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Anne Semamba Makinda, akohojiwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Fedha, Bw. Benny Mwaipaja (kushoto) katika kipindi maalumu cha Sabasaba cha Hazina TV baada ya kutembelea Banda la Wizara hiyo katika Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yanayofanyika katika viwanja vya Julius Nyerere, Temeke, jijini Dar es Salaam.
Kamisaa wa Sensa na Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Anne Semamba Makinda, akiagana na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Fedha, Bw. Benny Mwaipaja, baada ya mahojiano ya kipindi maalumu cha Sabasaba cha Hazina TV baada ya kutembelea Banda la Wizara hiyo katika Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba), jijini Dar es Salaam, ambapo alisisitiza matumizi ya takwimu sahihi.

Mhe. Makinda ametoa rai hiyo alipotembelea Banda la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yanayofanyika katika viwanja vya Julius Nyerere Barabara ya Kilwa, Temeke, jijini Dar es Salaam, ambapo amesisitiza matumizi ya Takwimu sahihi kwa maendeleo.
Kamisaa wa Sensa na Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Anne Semamba Makinda, akizungumza na vyombo vya Habari kuhusu umuhimu wa sensa iliyofanyika ambayo inasaidia katika kupanga mipango ya maendeleo, alipotembelea Banda la Wizara hiyo katika Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba), jijini Dar es Salaam.
Afisa Habari Mwandamizi wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Fedha, Bw. Ramadhani Kissimba, akimuongoza Kamisaa wa Sensa na Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Anne Semamba Makinda, kutembelea Banda la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yanayofanyika katika viwanja vya Julius Nyerere Barabara ya Kilwa, Temeke, jijini Dar es Salaam, ambapo amesisitiza matumizi ya Takwimu sahihi kwa maendeleo.
Kamisaa wa Sensa na Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Anne Semamba Makinda, akisaini kitabu cha wageni alipotembelea Banda la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba), jijini Dar es Salaam, katikati ni Afisa Habari Mwandamizi kutoka Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Fedha, Bw. Ramadhani Kissimba na kushoto ni Mwandishi Mwendesha Ofisi wa Kitengo hicho, Bi. Masia Msuya.
Kamisaa wa Sensa na Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Anne Semamba Makinda, akipewa maelezo ya Mfumo wa Kielektroniki wa Malipo ya Serikali (GePG) na Afisa Usimamizi wa Mifumo ya Fedha kutoka Idara ya Usimamizi wa Mifumo ya Fedha Wizara ya Fedha, Bw. Emmanuel Maendaenda, alipotembelea Banda la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba), jijini Dar es Salaam.
Kamisaa wa Sensa na Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Anne Semamba Makinda, akipewa maelezo ya elimu ya fedha kwa wananchi hususani vijijini na Maafisa waandamizi kutoka Idara ya Uendelezaji Sekta ya Fedha kutoka Wizara ya Fedha, alipotembelea Banda la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba), jijini Dar es Salaam.

Amesema, takwimu zilizotokana na sensa zina kila kitu hivyo ni vyema zikatumika kikamilifu katika mipango ya maendeleo lakini pia kutumiwa na watafiti wakiwemo wa vyuo mbalimbali katika kupata majibu ya changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii.
Kamisaa wa Sensa na Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Anne Semamba Makinda, akipewa maelezo kuhusu usimamizi wa madeni kutoka kwa Mchumi Mwandamizi, Idara ya Usimamizi wa Madeni Wizara ya Fedha, Bw. Sepo Seni, alipotembelea Banda la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba), jijini Dar es Salaam.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha).

Amewataka wananchi kutembelea Banda la Wizara ya Fedha ili kupata elimu ya zianda kuhusu Sensa na takwimu kwa kuwa sasa Ofisi ya Takwimu inafanyakazi ya kutoa elimu kwa umma kuhusu matokeo ya Sensa iliyofanyika.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news