Serikali yatenga fedha ujenzi wa Daraja la Lumecha

RUVUMA-Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu),Mhe. Jenista Mhagama ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Peramiho ameelekeza Wakala wa Barabara za Vijijini na Mjini (TARURA) Halmashauri ya Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma kuhakikisha Daraja la Lumecha linajengwa ndani ya kipindi kifupi na kwa ubora.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Mhe. Jenista Mhagama (Mb) akizungumza na wananchi wa Liweta katika mkutano wa hadhara kuhusu ujenzi wa Daraja la Lumecha unatarajia kuanza hivi karibuni.

Waziri ametoa kauli hiyo Julai 10,2024 wakati wa ziara yake ya kutembelea miradi ya maendeleo katika Kijiji cha Liweta Halmashauri ya Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama (Mb) akikagua ujenzi wa godauni linaoendelea kujengwa ambalo litatumika kama soko la mazao katika kijiji cha Mpandangindo wakati wa ziara yake katika Kata ya Mapandangindo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Mhe. Jenista Mhagama (Mb) akikagua ujenzi wa jengo la msikiti linaloendelea kujengwa katika Kijiji cha Mpandangindo na kuahidi kutoa mchango wa bati mia moja kwa ajili ya kupaua.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama (Mb) ametembelea zahanati ya Litulo na kutoa fedha kiasi cha Milioni moja kwa ajili ya kuanza ujenzi wa kichomea taka katika zahanati hiyo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama (Mb) ametembelea nyumba ya Mtambo (House Pump) iliyopo Liagila wakati wa ziara yake katika kata ya Mpandangindo.

“Serikali imetoa kiasi cha shilingi milioni 400 kujenga madaraja na akiba ya fedha itakayobaki itatumika kutengeneza barabara mpaka Kijiji cha Liweta ikiwa ni pamoja na kufukia shimo lilopo katika barabara hiyo."

Amesema, kazi ya ujenzi wa barabara ni kazi muhimu, "naomba wananchi msaidie katika kulinda mradi ili ujenzi ukamilike kwa wakati na tufungue njia zitakazochochea uchumi katika Kijiji cha Liweta."

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news