Shilingi Milioni 115 kujenga Kituo cha Polisi katika Kijiji cha Bashnet

MANYARA-Zaidi ya shilingi milioni 115 zitatumika kujenga Kituo cha kisasa cha Polisi katika Kijiji cha Bashnet Wilayani Babati ili kukidhi haja ya kusogeza Huduma za kipolisi kwa Wananchi.
Hayo yamesemwa Julai 23, 2024 na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini Mhe. Daniel Sillo, katika muendelezo wa ziara yake ya Kiserikali ya Kijiji kwa Kijiji, Kata kwa Kata, Kitongoji kwa Kitongoji katika Jimbo la Babati Vijijini akisikiliza na kutatua kero mbalimbali za Wananchi.
Mhe. Sillo amesema Kituo hicho kitajengwa katika eneo ambalo Serikali ya Kijiji itatenga.

Ombi hilo la Wananchi wa Kijiji hicho kupatiwa Kituo cha Polisi limekuja kutokana na ukweli kwamba Kijiji cha Bashnet kinakua kwa kasi hivyo upo uwezekano mkubwa wa kuongezeka kwa matukio ya kihalifu sambamba na kufuata Huduma hiyo kwa umbali mrefu.

Katika ziara hiyo Mhe. Sillo ameambatana na wataalam mbalimbali kutoka sekta ya elimu, afya, miundombinu na nishati ili kutoa ufafanuzi na majibu ya hoja mbalimbali za wananchi.
Pia katika ziara yake Mhe. Sillo ameambatana na Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Babati ikiongozwa na Mwenyekiti wa CCM, Jackson Hhaibey.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news