Sillo awasili wilayani Ngara kwa ziara ya kikazi

KAGERA-Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Daniel Sillo (Mb) amewasili Wilayani Ngara Mkoani Kagera kufanya ziara ya kikazi ambapo amepokelewa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Ngara Bi. Hatujuani Lukari kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya leo Julai 29, 2024.
Mhe. Sillo amepokelewa pia na Mbunge wa Jimbo la Ngara, Mhe. Ndaisaba Ruhoro, Kamishna wa Huduma za Urekebu wa Jeshi la Magereza (CP) Bertha Minde, Wataalam kutoka Sekta mbalimbali pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Ngara.
Katika ziara hiyo, Naibu Waziri Sillo atapokea taarifa ya hali ya usalama Wilayani humo, atakagua eneo la Shamba la Jeshi la Magereza pamoja na kufanya mkutano wa hadhara.

Mbunge Ndaisaba amemshukuru Naibu Waziri Sillo kwa kutimiza ahadi yake ya kufanya ziara katika Jimbo hilo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news